MICHUZI: ZAIDI YA WANAWAKE 7500 WANUFAIKA NA "MWEI" MKOANI MOROGORO

MICHUZI
Libeneke la Globu ya Jamii 
thumbnail ZAIDI YA WANAWAKE 7500 WANUFAIKA NA "MWEI" MKOANI MOROGORO
Jul 28th 2013, 09:35, by noreply@blogger.com (MUHIDIN MICHUZI)

Baadhi ya wanawake wajasiriamali wadogowadogo wa Tarafa ya Matombo Morogoro vijijini wakipatiwa elimu na wafanyakazi wa Vodacom Tanzania hawapo pichani,kabla ya kupatiwa mikopo yao ya pesa isiyokuwa na riba ya zaidi ya shilingi Milioni 327 iliyotolewa na Vodacom Tanzania kupitia mradi wake wa "MWEI".mikopo hiyo inawawezesha wanawake wajasiriamali wadogowadogo nchini kujiendeleza katika biashara zao,na kurudisha mikopo hiyo kwa njia ya M-PESA.
Mwenyekiti wa kikundi cha tupendane Bi. Rosena Rashid -Mkazi wa Tarafa ya Matombo Morogoro vijijini akisaini kitabu cha orodha ya wakina mama wajasiriamali wadogowadogo waliokuwa wakipatiwa mikopo ya pesa isiyokuwa na riba ya zaidi ya shilingi Milioni 327 toka Vodacom Tanzania kupitia mradi wake wa "MWEI"unaowawezesha wanawake wajasiriamali wadogowadogo nchini, na kurudisha mikopo hiyo kwa njia ya M-PESA.anaeshuhudia kushoto ni Meneja Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Bi.Rukia Mtingwa.
Mwenyekiti wa kikundi cha tupendane Bi.Rosena Rashid- Mkazi wa Tarafa ya Matombo Morogoro vijijini akipokea mkopo wa pesa kutoka kwa wakala wa M-PESA wa Vodacom Morogoro,Bw.Verus Bitahilo(alieketi)Kampuni hiyo inatoa mikopo kwa wanawake wadogowadogo wajasiriamali hapa nchini isiokuwa na riba wanawake hao walipokea mkopo huo yenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 327 kupitia mradi wake wa "MWEI" na kurudisha mikopo hiyo kwa njia ya M-PESA.anaeshuhudia wapili toka kulia walioketi ni Meneja wa mradi huo Bi.Grace Lyon.
Mwenyekiti wa kikundi cha Mother support Bi.Veronica Nyemele- Mkazi wa Tarafa ya Matombo Morogoro vijijini akionesha na kufurahia pesa zake alizopewa mkopo usio na riba toka Vodacom Tanzania kupitia mradi wake wa "MWEI"unaowawezesha wanawake wajasiriamali wadogowadogo nchini, wanawake 7500 walinufaika na mkopo huo wa zaidi ya shilingi Milioni 327.
Sehemu ya wanawake wajasiriamali wadogowadogo walionufaika na mkopo huo wa zaidi ya shilingi Milioni 327.

You are receiving this email because you subscribed to this feed at blogtrottr.com.

If you no longer wish to receive these emails, you can unsubscribe from this feed, or manage all your subscriptions
Previous
Next Post »